Wednesday, 9 September 2015


Image copyrightRays


Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza ametimiza miaka 63 katika enzi.
Huo ni muda mrefu zaidi katika historia ya Uingereza.Alitawazwa kuwa malkia akiwa na umri wa miaka 25 pekee.

Image captionAlipotawazwa

Mara ya kwanza alipofahamishwa kuwa ndiye atakayekuwa malkia wa Uingereza alikuwa nchini Kenya .

Image copyright
Image captionAkiwa na mumewe

Alikuwa katika ziara rasmi nchini Kenya akiwa na mmewe Philip wakati huo akiwa na umri wa miaka 25 pekee.

Image captionMalkia Elizabeth

Walikuwa wakikaa katika hoteli ya Treetops na jioni moja ikatangazwa kuwa babake amefariki akiwa usingizini.

Image copyrightRays
Image captionMalkia Elizabeth ofisini

Na hapo akawa Malkia lakini hakuambiwa habari hizo hadi alasiri siku iliyofuata.

Image copyrightRays
Image captionMalkia Elizabeth anawapenda mbwa

Mmewe alimpeleka katika ikulu ndogo ya Sagana na kumpa habari kwamba sasa ndiye malkia wa Uingereza.


Sasa miaka 63 baadaye Malkia anawashukuru sana wote waliomtumia ujumbe wa heri njema.

Image copyrightPA
Image captionMalkia Elizabeth akipokea salamu


Image copyrightRays
Image captionMalkia akiwa na mumewe Prince Phillip

Akizungumza karibu na mpaka wa Scotland Malkia Elizabeth 89 alisema ni heshima kubwa kwake kuendelea kuwahudumia waingereza.

Image captionMalkia Elizabeth ameweka rekodi ya kutawala kwa kipindi kirefu zaidi cha miaka 63

Malkia Elizabeth amehudumu kwa siku 23,226 , yaani miaka 63 .

Image copyrightRays
Image captionMalkia Elizabeth amehudumu kwa siku 23,226
Image copyrightrays
Image captionViongozi wengi wamesifu kwa unyenyekevu wake


Categories:

0 comments:

Post a Comment