Tuesday, 19 January 2016

Moto umetokea katika ghorofa ya juu zaidi ya hoteli ya kifahari ya Ritz mjini Paris nchini Ufaransa.
Hakuna majeruhi yaliyoripotiwa na msemaji wa huduma za moto anasema kuwa jambo muhimu ni kuuzuia moto huo kusambaa
Hoteli ambayo ndimo alilala mwana mfamle wa uingereza Diana usiku wa mwisho kabla akufe kwenye ajali ya barabarani ilikuwa imefungwa kufanyiwa ukarabati na hakuna mgeni alikuwa akiishi humo.
Princes Diana alikuwa akiishi katika hoteli hiyo wakati alikufa mwaka 1997 akiea na mpenzi wake Dodi Al Fayed, ambaye mtoto wa mmiliki wa hoteli hiyo bilionea raia wa misri Mohamed al Fayed.
Ilikuwa ifunguliwe baadaye mwaka huu baada ya kufungwa kwa miaka mitatu ili kufanyiwa ukarabati.
PolisiPolisi nchini Kenya wamenasa noti bandia za jumla ya $693m (£485m) baada ya kufanya msako katika nyumba moja jijini Nairobi.
Watu wawili, mmoja kutoka Cameroon na mwingine kutoka Niger, wamekamatwa kuhusiana na pesa hizo.
Mkuu wa polisi Joseph Boinett akitangaza kupatikana kwa pesa hizo, amewaambia wanahabri kwamba hicho ni “kiasi kikubwa sana” cha pesa.
Amesema noti bandia za euro 369 milioni pia zimepatikana, pamoja na mitambo ya kutengeneza noti bandia.
Polisi walifanya msako baada ya kupokea habari za mfanyabiashara aliyetapeliwa Sh40 milioni za Kenya baada ya kuhadaiwa kwamba zingeongezwa mara tatu na kuwa Sh120 milioni.
Kwa jumla, pesa hizo zilizopatikana katika mtaa wa South C, zikibadilishwa na kuwa shilingi za Kenya zinafikia Sh110 bilioni ambazo ni sawa na shilingi trilioni 2.3 za Tanzania.
Umoja wa Mataifa na mashirika ya kutoa misaada yametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuipa msaada wa takriban dola 885 milioni kuwasaidia zaidi ya watu milioni tano wanaohitaji misaada ya chakula nchini Somalia.
Miongoni mwao wakiwa zaidi ya watoto 310,000 ambao wanakabiliwa na tishio kubwa na kuangamia kutokana na baa la njaa na utapia mlo ikiwa hawatapata misaada ya dharura.Shughuli za kusambaza misaada zimeathirika pakubwa kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha, usalama na mvua ya el nino inayoendelea kushuhudiwa katika sehemu kadhaa.
Mratibu wa umoja wa mataifa anayehusika na masuala ya misaada ya kibinadamu nchini Somalia Peter De Clrecq, amesema wito huo ni muhimu sana na utasaidi watu wengine milioni moja nukta moja waliokimbia vita nchini Somalia.
Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi ni pamoja na Baido, Bossaso, Gaalkayo, Kiismayo na mji mkuu wa Mogadishu.

Monday, 18 January 2016




















Suleiman Said Suleiman wakati wa uhai wakeSuleiman Said Suleiman Wakati wa Uhai wake.

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), Suleiman Said Suleiman amefariki dunia akiwa katika mazoezi ya kuogelea katika Bahari ya Hindi, eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mauti yalimkuta jana asubuhi baada ya kukosa nguvu wakati akiwa anaogelea.
Mkurugenzi wa Sheria wa TAA anayeshughulikia pia Uhusiano, Ramadhan Maleta, alisema ilikuwa ni kawaida ya Suleiman kufanya mazoezi ya mwili kila siku kabla ya kwenda kazini.
Alisema jana kati ya saa 12:00 na saa 1:00 asubuhi, akiwa anaogelea mmoja wa aliokuwa ameongozana nao, aligundua kuwa amekosa nguvu akiwa majini.
“Akaanza kumsaidia akiwa na wenzake ambao waliomba msaada kumtoa majini lakini wakagundua kuwa alikuwa ameshapata athari,” alisema Maleta.
Alisema walimkimbiza Hospitali ya Aga Khan kwa ajili ya kupatiwa matibabu lakini kabla ya kufika walibaini kutokuwa na uhai.
Maleta alisema wafanyakazi wa TAA kwa ujumla wanasikitika kutokana na msiba huo, kwani Said alikuwa mtu wa mfano mwenye utaalamu wa viwanja vya ndege akiwa mhandisi mwenye ujuzi mkubwa.
Alisema alikuwa kiongozi mwenye upendo asiyekuwa na majivuno na kutokana na kuwa na roho nzuri na ukaribu na wafanyakazi, aliwatambua wafanyakazi wote wa TAA nchi nzima kwa majina.
Maleta alisema Mkurugenzi huyo ametumikia TAA kuanzia miaka ya 1970, akisimamia miradi mbalimbali ya uimarishaji na uboreshwaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini.
Alisema atakumbukwa daima kwa upanuzi wa uwanja wa Terminal 3.
Alisema katika ujenzi huo, alifanikisha kumaliza utata na kuhakikisha anapatikana mkandarasi ambaye amewezesha ujenzi kufikia mahali pazuri. Kwa mujibu wa Maleta, Suleiman ameacha mjane na watoto watatu.
Buyelakhaya Dalindyebo.
Mfalme wa aba Thembu nchini Afrika Kusini anayehudumia kifungo jela Buyelakhaya Dalindyebo amelazwa hospitalini mashariki mwa London akiugua ugonjwa usiojulikana,kulingana na ripoti za vyombo vya habari nchini Afrika Kusini.
Hii ni mara ya pili kwa yeye kulazwa hospitalini katika kipindi cha wiki za hivi karibuni baada ya mfalme huyo kupelekwa katika hospitali moja nchini humo alipofanya mgomo wa kula.
Ripoti hizo zilisema kwamba anaugua vidonda vya tumbo na shinikizo ya akili.
Kulingana na gazeti la the New Age,idara ya kurekebishia watu tabia imesema kuwa hali yake ilizorota mda mchache tu baada ya kutakiwa kuondoka hospitalini.
Mfalme Dalindyebo anatoka katika ukoo wa aba Thembu pamoja na aliyekuwa rais wa taifa hilo Marehemu Nelson Mandela.
Alianza kuhudumia kifungo chake cha miaka 12 jela kwa utekeji nyara,unyanyasaji na kuchoma nyumba moto baada ya harakati za kujaribu kufutilia mbali hukumu hiyo.
Kesi dhidi yake inahusiana na mgogoro wa miongo miwili aliokuwa nao na wafuasi wake.
Donald Trump.
Wabunge wa Uingereza wamekuwa na mjadala kuhusu kupigwa marufuku au la kwa anayewania nafasi ya kupeperusha bendera ya chama cha republican katika kinyang'anyiro cha urais wa Marekani, Donald Trump kuingia nchini Uingereza.
Mjadala huo uliochukua muda wa saa tatu umekuja baada ya karibu nusu milioni ya watu nchini Uingereza kuunga mkono hatua ya kumzuia Trump kuingia Uingereza. baada ya Trump kusema kuwa Waislamu wote wazuiwe kuingia marekani ikiwa ni njia ya kupambana na vitendo vya kigaidi
Wabunge hata hivyo hawakuonyesha shauku kubwa ya kumfungia milango Trump ili asiingie Uingereza kwani hakuna kura yeyote iliyopigwa mwishoni mwa mjadala
Mmoja wa wabunge wa Uingereza ambaye ni muislamu amesema kauli za Trump ni sumu, huku msemaji wa idara ya mambo ya ndani Jack Dromey akisema kuwa Trump azuiwe kuingia Uingereza.
Wakati huo huo Trump ameendelea na kampeni zake, akizungumza katika chuo cha Liberty, chuo binafsi cha kikristo kilicho Lynchburg, Virginia amewaambia wanafunzi wa kikristo kuwa wanapaswa kuungana kuilinda dini yao.
''Tunapaswa kuilinda kwa kuwa kuna mambo yanafanyika, mambo mabaya sana, sijui ni nini lakini hatuungani labda.dini nyingine wanaungana kuzuia, hapa tunayo...ukitazama nchi hii, asilimia 70 mpaka 75 ni wakristo, watu wengine wanasema hata zaidi ya hiyo, inadhihirisha nguvu tuliyonayo, tunapaswa kuungana'' alieleza Trump katika kampeni yake.
Baadhi ya Maeneo yalioathiriwa na Mvua.
Takriban watu watatu wameuwa na wengine sita kujeruhiwa baada ya kushuhudiwa mvua kubwa jana usiku katika wilaya ya Mutambua karibu na mji mkuu wa Burundi Bujumbura.
Radio ya taifa ya nchini humo ilitangaza kuwa karibu nyumba 90 ziliharibwa.
Pia barabara inayoelekea katika bwawa la kuzalisha umeme katika eneo hilo nayo iliharibiwa.
Kila kunapotekea mvua kubwa nchini Burundi mji mkuu Bujumbura na vitongoji vyake hukubwa na mafuriko ambavyo huchangia kutokea kwa maporomoko ya udongo na kisha maafa.
Zaidi ya wahamiaji haramu themanini , raia wa Ethiopia wamekamatwa na polisi Tanzania wakiwa safarini kwenda mji wa Mbeya kusini mwa nchi hiyo.
Wengi wa wahamiaji hao walikuwa katika hali mbaya wengi wakiwa hawana maji mwilini,kulingana na kamanda wa polisi Peter Kakamba.
''Baada ya kuwakamata tulilazimika kuwatafutia wauguzi ili wawekwe maji mwilini,walikuwa na njaa,na wasiojiweza,walikuwa wamelaliana katika lori hilo,tuliwapatia huduma ya kwanza na kuwalisha uji kabla ya kuwaleta Iringa mjini''.
Tanzania na Malawi hutumiwa kama vituo muhimi vya watu wanaotoroka kiangazi na migogoro nchini Ethiopia na Somalia ili kuweza kufika Afrika Kusini.

Germain Katanga.
Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo inasema kuwa inataka kumfungulia mashtaka kiongozi wa waasi Germain Katanga ambaye tayari amehukumiwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.
Katanga alikuwa akitumikia kifungo chake gerezani katika mjini Kinshaha na alikuwa aachiliwe hii leo.
Waaziri wa haki nchini DRC Alexis Thambwe Mwamba aliliamba shirika la habari la AFP kuwa Katanga hawezi kuachiliwa.
Anatakikana nchini Jamhuri wa kidemokrasi ya Congo kwa uhalifu tofauti wa kivita na ule uliotumiwa kumhukumu kwenye mahakama ya ICC.
Mwezi uliopita shirika la haki za binadamu lenye makao yake nchini Marekani lilisema kuwa Katanga anatakikana kwa uhalifu uliotendwa mwaka 2005 na kutaka kesi yake ifanyike kwa haraka.

Sunday, 17 January 2016







 







Wanajeshi Waliojeruhiwa mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege.
Wanajeshi wa Kenya waliojeruhiwa kwenye shambulio lililofanywa na wapiganaji wa Al-Shabab eneo la el-Ade wamesafirishwa hadi Nairobi.
Wapiganaji hao wa Al-Shabab walishambulia kambi ya jeshi la Umoja wa Mataifa nchini Somalia na kuna ripoti kuwa wanajeshi kadhaa wa Kenya waliuawa huku wengine wakijeruhiwa.
Idadi ya wanajeshi waliouawa haijabainika wazi lakini kundi hilo la Al shabaab linadai kuwa liliwauwa zaidi ya wanajeshi sitini madai ambayo serikali ya Kenya imekanusha.Mwanajeshi aliyejeruhiwa akiwa anapakizwa katika gari ya Wagonjwa.
Miongoni mwa waliokuwa kwenye uwanja wa ndege wa Wilson kuwalaki wanajeshi hao waliojeruhiwa ni pamoja na waziri wa ulinzi Bi Rachael Omamo na maafisa wengine wa ngazi ya juu jeshini na serikalini.
Omamo amesema habari kuhusu wanajeshi walioangamia zitawasilishwa kwa familia zao moja kwa moja.
Aidha amesema wanajeshi wa Kenya bado wangali wanapambana na wapiganaji hao wa Al shabaab ili kujaribu kuwakomboa wanajeshi waliokwama ikiwa wapo.Kenya imekariri kuwa haitaondoa wanajeshi wake Somalia hadi pale kundi hilo la al shabaab litakaposambaratishwa kabisa na amani kurejea nchini humo.
Wakati huo huo kundi hilo limedai kuwa linawashikilia wanajeshi kadhaa wa Kenya mateka.
Al Shabaab limesema ni mara ya kwanza kikosi chake maalum cha Saleh ali saleh Nabhan kilifanya shambulio ndani ya somalia.Waziri wa Ulinzi Nchini Kenya akihutubia vyombo vya Habari.
Saleh ali Saleh Nabhan alikuwa kiongozia wa Al qaeda katika kanda ya Afrika mashariki na aliuawa kwenye shambulio lililofanywa na Marekani mwaka wa 2008
Tangu mwaka wa 2011 wakati Kenya ilituma wanajeshi wake nchini Somalia, kundi hilo limefanya mashambulio kadhaa ya kigaidi nchini Kenya na kusababisha maafa makubwa.