Thursday, 27 August 2015


                                  
WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA MWAKA 2014, KIDATO CHA NNE MWAKA 2014
NA JKT MWAKA 2015 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA JESHI LA POLISI
UTANGULIZI:
Jeshi la polisi Tanzania linawajulisha kwamba litaendesha mafunzo ya awali ya Jeshi la
Polisi  kwa  miezi  tisa  katika  shule  ya  Polisi  Tanzania  “Moshi”  kuanzia  taerehe
29/08/2015. Mafunzo hayo yatahusisha wahitimu wa vyuo vikuu, kidato cha sita kidato
cha nne wote wa mwaka 2014. Aidha wahitimu wa Jeshi la kujenga Taifa wa mwaka
2015 watahusika pia.
Maelekezo Muhimu.
1.  Waliochaguliwa  watatakiwa   kuripoti  kwa  makamanda  wa  Polisi  wa  Mikoa  Tarehe
28/08/2015 kwa ajili ya maandalizi ya usafiri wa kwenda shule ya Polisi Tanzania
tarehe  29/08/2015  kila  mmoja  atatakiwa  kuwa  na  nauli   ya   kumwezesha  kusafiri
toka  makao  makuu  ya  mkoa  anakoanzia  kusafiri  hadi  shule  ya  Polisi  Moshi  na
atarejeshewa nauli atakapofika chuoni baada ya kuwasilisha Tiketi ya safari.
2.  Tarehe ya mwisho ya kuripoti chuoni ni tarehe 5/09/2015 na atakayeripoti baada ya
hapo hatapokelewa
3.  Vijana hawa watalazimika kufika shuleni wakiwa na vitu vifuatavyo :
a)  Vyeti vyao vyote vya masomo( original Academic Certificates/Result slip pamoja
na Leaving certificates) kidato cha Nne, Sita na vyuo. Vyeti halisi vya kuzaliwa
(Original Birth certificates). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.
b)  Mashuka mawili rangi ya Bluu bahari (light blue)
c)  Chandarua chenye upana futi tatu
d)  Nguo za michezo(Track suit nyeusi,Tshirt blue naRaba)
e)  Pasi ya Mkaa.
f)  Ndoo moja.
g)  Pesa  za  kulipia  bima  ya  afya  kiasi  cha  shilingi  elfu  hamsini   na  mia  nne  tu
(50,400/=).
h)  Pesa kidogo ya kujikimu.
4.  Kwa mujibu wa kanuni za shule ya Polisi ni marufuku kufika shuleni na simu ya
mkononi. Atakayepatikana na simu atafukuzwa shuleni hapo. Shule itaelekeza na
kusaidia kufanya mawasiliano.
5.  Orodha ni kama ilivyo hapa hini:- KUANGALIA MAJINA YOTE BONYEZA HAPA
Categories:

0 comments:

Post a Comment