Wednesday, 26 August 2015


Rais Bashar al-Assad, amesema ana imani licha ya tuhuma kwamba Iran na Urusi huenda zikamtenga kutoa nafasi ya makubaliano kufuatia makubaliano ya nyuklia ya Iran na mataifa ya magharibi.
Licha ya shughuli nyingi za kidiplomasia katika eneo hilo kufuatia makubaliano hayo, Assad amesema hakuna dalili ya makubaliano ndani ya Syria, na amemshutumu mumbe maalum wa kimataifa wa amani kwa kuwa na upendeleo.
Katika mahojiano marefu na yasiokuwana ushindani, katika kituo cha televisheni cha Lebanon - al Manar inayoendeshwa na washirika wake wa Hezbollah, Rais Assad alitaja nafasi zilizopo ambazo hazijabadilika licha ya hali duni inayovikabili vikosi vyake katika vita.


Jitihada za kidiplomasia zimeshinikizwa baada ya makubaliano hayo na Iran ya nyuklia, na kusababisha uvumi kwamba huenda kukawa na muafaka wa Syria.
Lakini rais Assad amesema kwamba hakuna uwezekano wa kufikiwa suluhu.Na ili hilo liweze kufanyika, basi wale aliowataja kuunga mkono "ugaidi" - akimaanisha Saudia Waturuki na wengine - itabidi wasite kufanya hivyo.


Suluhu yoyote ni lazima itokane kwanza na vita dhidi ya ugaidi.
Ameeleza imani yake kwa Urusi na Iran ambao amezitaja nchi hizo kutowatenga rafiki zake tofauti na Marekani.
Na iwapo Iran itaibuka na nguvu zaidi kutokana na makubaliano ya nyuklia, amesema hilo litakuwa na faida kwa washirika wake Syria.

0 comments:

Post a Comment